yegowasutelevision

yegowasutelevision kutoa habari za uhakika Kila zinapochipuka

🔥 MOTO WAKUMBA HIFADHI YA KILIMANJARO, WAZIRI KIJAZI ASEMA UMEDHIBITIWA KWA 90%Moshi/Tanzania — Moto umezuka katika Hifa...
05/09/2026

🔥 MOTO WAKUMBA HIFADHI YA KILIMANJARO, WAZIRI KIJAZI ASEMA UMEDHIBITIWA KWA 90%

Moshi/Tanzania — Moto umezuka katika Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro, huku Serikali ikisema kuwa jitihada za kuudhibiti moto huo zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa na kufikia asilimia 90.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, ametembelea eneo lililoathirika siku ya Jumamosi kwa ajili ya kutathmini hali ya moto huo pamoja na hatua zinazochukuliwa na mamlaka kuuzima kabisa.

Akizungumza baada ya kutembelea eneo hilo, Kijaji alisema kuwa moto huo tayari umedhibitiwa kwa asilimia 90, huku akieleza kuwa juhudi za kuuzima sehemu iliyobaki zikiendelea.

Alisema chanzo cha moto huo bado hakijafahamika na kwamba uchunguzi unaendelea kubaini kilichosababisha moto huo.

«“Jitihada za kuuzima moto huo kabisa zinaendelea na tunatarajia kuwa sehemu iliyobaki itazimwa kabla ya mwisho wa leo (Jumamosi),” alisema Kijaji.»

Moto ulianzia Kikerelwa

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, moto huo ulianza kuwaka Alhamisi majira ya saa 9:30 alasiri, sawa na saa 15:30 kwa saa za Afrika Mashariki, katika eneo la Kikerelwa, upande wa kaskazini mashariki mwa Mlima Kilimanjaro, Wilaya ya Rombo.

Tukio hilo limeibua tahadhari kutokana na umuhimu wa eneo hilo kwa uhifadhi wa mazingira, misitu na shughuli za utalii.

Waziri Kijaji amewataka wakazi wanaoishi karibu na hifadhi hiyo kuwa makini na kuepuka shughuli zinazoweza kusababisha moto, akisisitiza umuhimu wa kulinda mazingira pamoja na wanyamapori.

Si mara ya kwanza Kilimanjaro kukumbwa na moto

Moto huu si tukio la kwanza kutokea katika eneo la Mlima Kilimanjaro.

Septemba 2023, moto uliendelea kuwaka kwa takribani wiki moja na kuharibu eneo lenye ukubwa wa takribani kilomita za mraba 17, sawa na karibu asilimia moja ya eneo la hifadhi ya mlima huo.

Aidha, mwaka 2022, moto mwingine uliendelea kwa takribani mwezi mmoja na kusababisha uharibifu wa maelfu ya hekta za msitu unaozunguka mlima huo.

Matukio hayo yameendelea kuongeza umuhimu wa kuchukua hatua za haraka za kuzuia na kudhibiti moto katika maeneo ya hifadhi, hasa katika kipindi ambacho mazingira yanaweza kuwa katika hatari ya kushika moto.

Kilimanjaro ni hazina ya utalii Tanzania

Mlima Kilimanjaro ni miongoni mwa vivutio vikubwa na maarufu vya utalii nchini Tanzania. Ukiwa na urefu wa karibu mita 5,900 kutoka usawa wa bahari, mlima huo huvutia maelfu ya watalii kutoka sehemu mbalimbali duniani wanaofika nchini kwa ajili ya kupanda mlima na kushuhudia mandhari yake.

Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro pia ina umuhimu mkubwa katika uhifadhi wa misitu, bioanuwai na mazingira yanayozunguka mlima huo.

Serikali na mamlaka za uhifadhi sasa zinaendelea na juhudi za kuhakikisha moto uliobaki unazimwa kabisa, huku uchunguzi ukiendelea kubaini chanzo cha tukio hilo.

TRA SACCOS YATOA PONGEZI NYAIROMA SHULE YA MSINGI, YAZINDUA TRA CLUB; YATOA VITI NA TAULO ZA K**E KWA WANAFUNZISIRARI, M...
04/09/2026

TRA SACCOS YATOA PONGEZI NYAIROMA SHULE YA MSINGI, YAZINDUA TRA CLUB; YATOA VITI NA TAULO ZA K**E KWA WANAFUNZI

SIRARI, MARA — Septemba 2, 2026: Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha TRA SACCOS kimeendelea kuunga mkono juhudi za kuboresha elimu katika Shule ya Msingi Nyairoma, Sirari, kwa kutoa mchango wa vifaa mbalimbali kwa shule hiyo pamoja na kuzindua TRA Club.

Mchango huo umetolewa katika Mahafali ya Darasa la Saba kwa mwaka 2026 yaliyofanyika shuleni hapo, ambapo wadau mbalimbali walishiriki katika kupongeza wanafunzi waliohitimu pamoja na kujadili namna ya kuimarisha mazingira ya elimu.

Pamoja na mambo mengine, TRA SACCOS imetoa viti vya kukalia kwa matumizi ya wanafunzi, ikiwa ni sehemu ya kusaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia shuleni.

Aidha, TRA SACCOS imetoa taulo za k**e kwa wanafunzi wa k**e, hatua inayolenga kuwasaidia wanafunzi hao kukabiliana na changamoto za hedhi wanapokuwa shuleni na kuhakikisha hawaathiriki katika mahudhurio na masomo yao.

Msaada huo umeelezwa kuwa muhimu katika kuwawezesha wanafunzi wa k**e kuendelea na masomo yao kwa kujiamini na bila kukumbwa na changamoto zinazoweza kuwafanya kukosa vipindi wakati wa hedhi.

Katika mahafali hayo, wazazi pia wamehimizwa kushirikiana na uongozi wa shule kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula wanapokuwa shuleni.

Imeelezwa kuwa chakula ni sehemu muhimu ya mazingira ya kujifunzia, kwani mwanafunzi anayepata chakula vizuri anakuwa na uwezo wa kuwa makini darasani na kufuatilia masomo yake kwa ufanisi zaidi.

Wazazi wametakiwa kujitokeza na kushiriki katika kuhakikisha watoto wao wanapata chakula shuleni, huku wakisisitizwa kuwa suala hilo ni jukumu la pamoja kati ya wazazi, shule na jamii.

Ujumbe umetolewa pia kwa wazazi kuhakikisha watoto wao wanahudhuria shule kwa wakati na kwa mwendelezo, pamoja na kushirikiana na walimu pale mtoto anapokuwa na changamoto inayoweza kusababisha kukosa masomo.

Katika hatua nyingine, TRA SACCOS imezindua TRA Club katika Shule ya Msingi Nyairoma.

Klabu hiyo inalenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa mapema kuhusu masuala ya kodi, uwajibikaji na umuhimu wa kodi katika maendeleo ya taifa.

Uzinduzi huo ni sehemu ya juhudi za kuwaandaa wanafunzi kuwa raia wenye maarifa, nidhamu, uwajibikaji na uelewa wa nafasi yao katika maendeleo ya taifa.

Katika hafla hiyo pia ilisisitizwa umuhimu wa kuendelea kuzingatia kaulimbiu ya Shule ya Msingi Nyairoma ya “Kazi na Michezo.”

Kaulimbiu hiyo inalenga kuwaandaa wanafunzi si kwa ufaulu wa darasani pekee, bali pia kuwajengea uwezo wa kufanya kazi, kushiriki michezo, kukuza vipaji, kuwa na nidhamu na kujenga mahusiano mazuri na jamii.

Lengo ni kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi wanakuwa na maarifa, ujuzi na maadili yatakayowawezesha kuwa raia wema na wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha.

Kwa kutambua mchango wa wadau mbalimbali katika maendeleo ya shule, uongozi wa Shule ya Msingi Nyairoma chini ya Mwalimu Mkuu Juma Ambali uliwapatia wadau hao vyeti vya pongezi.

Vyeti hivyo vimetolewa k**a ishara ya kuthamini mchango wa wadau katika kusaidia shughuli za shule, kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia pamoja na kuwawezesha wanafunzi kupata elimu katika mazingira bora.

Mahafali hayo yameonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, walimu, wazazi, walezi na wadau mbalimbali katika kuhakikisha watoto wanapata elimu bora.

Kwa upande wa TRA SACCOS, msaada wa viti na taulo za k**e, pamoja na uzinduzi wa TRA Club, umeongeza nguvu katika jitihada za shule kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira yanayowawezesha kusoma bila vikwazo na kujifunza kwa umuhimu wa kulipa kodi kwa hiari

Wadau wameendelea kusisitiza kuwa elimu ya mtoto ni jukumu la pamoja, hivyo wazazi na jamii kwa ujumla wanapaswa kuendelea kushirikiana na shule katika masuala ya chakula, mahudhurio, malezi, afya, usafi na maendeleo ya kitaaluma ya wanafunzi.

03/09/2026

BILA HAKI KUPATIKANA NIKUWA GEREZANI MUDA WOTE "LISSU"
TUANDIKIE MAONI YAKO JUU YA MSIMAMO HUO

NI GAZETI GANI LIMEKUVUTIA LEO USOME TUANDIKIE MAONI YAKO HAPO CHINI
31/08/2026

NI GAZETI GANI LIMEKUVUTIA LEO USOME TUANDIKIE MAONI YAKO HAPO CHINI

NI GAZETI GANI LIMEKUVUTIA LEO USOME TUANDIKIE MAONI YAKO HAPO CHINI Agosti 30, 2026 Pata kiungo Facebook X Pinterest Barua pepe Programu Nyingine   Pata kiungo Facebook X Pinterest Barua pepe Programu Nyingine Maoni Chapisha Maoni

HECHE AKAE MEZA MOJA NA WATAWALA LISSU AWE HURUViongozi wawili wa CHADEMA, Felix Mwembe na Barnabas Okola, wameeleza umu...
30/08/2026

HECHE AKAE MEZA MOJA NA WATAWALA LISSU AWE HURU
Viongozi wawili wa CHADEMA, Felix Mwembe na Barnabas Okola, wameeleza umuhimu wa kufanyika kwa mazungumzo na maridhiano kati ya viongozi wa CHADEMA na Serikali, wakimtaka Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, John Heche, kukaa meza moja na watawala ili kutafuta suluhu ya hali inayomkabili Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu.
‎

‎Kauli hizo zimekuja wakati kesi inayomkabili Lissu ikiendelea kuwa sehemu ya mjadala mkubwa wa kisiasa nchini, huku suala la namna ya kumaliza mvutano huo likizidi kujadiliwa ndani na nje ya CHADEMA.

‎

‎Kwa upande wake, Mwembe amesema kuna haja ya Heche kukaa pamoja na watawala na kuzungumza kuhusu maridhiano, akieleza kuwa mazungumzo yanaweza kuwa njia ya kutafuta suluhu na hatimaye kusaidia Lissu kuwa huru.

‎Mwembe anaamini kuwa badala ya kuendelea na mvutano, viongozi wanapaswa kutafuta nafasi ya kukutana na kujadiliana ili kuona namna ya kuvuka changamoto zilizopo.

‎

‎

‎Naye Barnabas Okola, Mjumbe wa CHADEMA Mkoa wa Morogoro, amesema chama hicho kinaamini kuwa kukutwa kwa Lissu na kesi ya kujibu si jambo linalopaswa kuwa lengo la msingi la harakati za chama.

‎

‎Okola amesema anaamini Lissu ana uwezo wa kuendelea kuongoza harakati za kisiasa, huku akieleza kuwa suala la kesi halipaswi kusababisha kusimama kwa harakati za chama.

‎

‎Aidha, Okola amegusia baadhi ya kauli zinazohusishwa na Lissu na ambazo, kwa mtazamo wake, zinafanana na kauli ambazo zimekuwa zikitolewa na Heche, lakini Heche hajakumbwa na hatua k**a hizo.

‎

‎Kutokana na hali hiyo, Okola amesisitiza umuhimu wa viongozi wa chama kutafuta njia ya mazungumzo na maridhiano badala ya kuendelea katika mvutano.

‎

‎Kwa pamoja, hoja zinazotolewa na Mwembe na Okola zinaelekeza kwenye wito mmoja — Heche kukaa meza moja na watawala kwa ajili ya mazungumzo na maridhiano, wakiamini kuwa njia hiyo inaweza kusaidia kutafuta suluhu ya mgogoro wa kisiasa unaozunguka Lissu.

‎

‎Wito huo sasa unaibua mjadala ndani ya siasa za Tanzania kuhusu k**a maridhiano yanaweza kuwa njia ya kumaliza mvutano na kufungua njia ya Lissu kuwa huru, au k**a suala hilo linapaswa kuachwa kwenye mchakato wa kisheria.

‎

‎Kwa sasa, kauli za Mwembe na Okola zinaongeza ‎Shinikizo kuhusu HECHE kwenye nafasi ya mazungumzo katika kutafuta suluhu ya changamoto zinazokikabili CHADEMA na viongozi wake.

CHACHA HECHE HAJAPOTEA ,MACHIRA AKANUSHA TAARIFA HIYO ASEMA IPUUZWEMwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA Mkoa wa Mar...
29/08/2026

CHACHA HECHE HAJAPOTEA ,MACHIRA AKANUSHA TAARIFA HIYO ASEMA IPUUZWE

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA Mkoa wa Mara, Alphonce Machira, amekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa Mwalimu Chacha Heche amepotea, akisema taarifa hizo hazina ukweli.

Machira amesema hadi leo Agosti 29, 2026, amekuwa pamoja na Mwalimu Chacha Heche katika shughuli mbalimbali, hivyo kuthibitisha kuwa kiongozi huyo yupo salama.

Akizungumza kwa njia ya simu kuhusu taarifa hizo, Machira amesema amepokea simu na jumbe nyingi kutoka kwa watu mbalimbali waliokuwa wakimuuliza kuhusu madai ya kupotea kwa Mwalimu Chacha Heche sio ya kweli.yaliyoonekana katika kurasa za Facebook watu wakizusha hizo taarifa huku akisisitiza kuwa kwa taarifa yeyote inayohusu kiongozi k**a mwalimu Chacha Heche ingiwekwa wazi na vyombo rasmi.

Amesema leo alikuwa Serengeti kwa ajili ya maandalizi ya ujio wa Makamu Mwenyekiti Chadema Taifa Mhe. John Wegesa Heche Septemba 9,2026 Serengeti, kabla ya kuelekea Nyamongo ambako kulikuwa na msiba wa mtoto wa mmoja wa wanachama wa kundi la Tarime Nguvu moja, ambalo Mwalimu Chacha Heche ni mwenyekiti.

Kwa mujibu wa Machira, Mwalimu Chacha Heche alikuwepo kwenye msiba huo akishiriki katika shughuli mbalimbali, ikiwemo kusimamia maandalizi ya chakula na kugawa chakula kwa waombolezaji.

Machira amesema baadaye alimuona Mwalimu Chacha Heche akiwa anaelekea kwenye shughuli za mazishi, huku yeye akiendelea kubaki Nyamongo.

«“Mwalimu Chacha Heche hajapotea, yupo. Leo mimi nilikuwa Serengeti kufanya maandalizi ya ujio wa Makamu Mwenyekiti. Baada ya hapo nikaenda Nyamongo ambako kulikuwa na msiba. Mwalimu Chacha Heche alikuwa pale k**a mwenyekiti wa Tarime Nguvu moja na alikuwa anasimamia shughuli za msiba,” amesema Machira.»

Ameongeza kuwa uwepo wa Mwalimu Chacha Heche Nyamongo pia ulihusishwa na maandalizi ya ujio wa Makamu Mwenyekiti unaotarajiwa kufanyika katika eneo hilo Septemba 10, 2026.

Machira amewataka wananchi kutokuwa na hofu kutokana na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii, akisema baadhi ya taarifa hizo zimekuwa zikidai kuwa Mwalimu Chacha Heche amepotea au antafutwa, jambo ambalo amesema si la kweli.

«“Mwalimu Chacha Heche yupo na mimi k**a Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA Mkoa wa Mara nathibitisha kwamba yupo. Leo tulikuwa naye Nyamongo. Hao wanaosambaza taarifa hizo wameamua kufanya mambo ya kijinga na kutaka kuleta taharuki,” amesema.»

Amesema endapo kutakuwa na jambo lolote linalomhusu Mwalimu Chacha Heche, taarifa sahihi itatolewa kupitia njia zinazofaa, badala ya wananchi kutegemea taarifa zisizothibitishwa zinazozagaa mitandaoni.

Machira amesisitiza kuwa kwa hali aliyokutana nayo mwenyewe leo, Mwalimu Chacha Heche yupo na anaendelea na shughuli zake k**a kawaida.

29/08/2026

LISSU CHANGIENI CHAMA CHA UKOMBOZI

28/08/2026

CHADEMA KUANZA MIKUTANO YAKE SEPTEMBA 9,2026
USISAHAU KUFOLLOW PAGE HII KWA HABARI ZAIDI

Leo agosti 28,2026 Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Mara, Mzee Charles Bullet, kwa niaba ya Mwenyekiti wa CHADEMA M...
28/08/2026

Leo agosti 28,2026 Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Mara, Mzee Charles Bullet, kwa niaba ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara, Mwl. Chacha Heche, amefanya kikao cha maandalizi ya mkutano wa chama unaotarajiwa kufanyika Mugumu, Wilaya ya Serengeti, Septemba 9, 2026.

Mkutano huo ambao awali ulipangwa kufanyika Septemba 4, 2026, umeahirishwa na kusogezwa mbele hadi Septemba 9, 2026, huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni majukumu ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa katika maandalizi hayo, John Heche anatarajiwa kutoa ushahidi katika kesi hiyo, jambo lililosababisha ratiba ya mkutano wa CHADEMA Mugumu kubadilishwa ili kuendana na majukumu hayo.

Katika kikao hicho, Mzee Charles Bullet amekutana na viongozi na wanachama kwa ajili ya kuweka mikakati ya maandalizi ya mkutano huo, ambao unatarajiwa kuwa sehemu ya shughuli za chama katika Mkoa wa Mara.

Mkutano huo wa Mugumu unatarajiwa kufanyika Septemba 9, 2026, baada ya ratiba ya awali ya Septemba 4 kubadilishwa.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPO CHINI KULINGANA NA TAARIFA YETU USISAHAU KUFOLLOW PAGE HII ✉️

Address

Musoma
Musoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when yegowasutelevision posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share