04/06/2026
π¨πππΌπππππ ππππ: MARSEILLE YAINGIA VITANI KUMNASA ISSAH CHOLE
Klabu kubwa ya soka ya nchini Ufaransa, Olympique de Marseille, imeibuka kuwa miongoni mwa vilabu vinavyoonyesha nia ya dhati ya kuwania saini ya kiungo mahiri wa Serengeti Boys, Issa M***a Chole, kufuatia kiwango chake cha kuvutia alichokionyesha katika michuano ya AFCON U-17 iliyofanyika nchini Morocco.
Taarifa kutoka barani Ulaya zinaeleza kuwa mabosi wa Marseille wamekuwa wakifuatilia kwa karibu maendeleo ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 16, ambaye ameendelea kujijengea jina kubwa kutokana na uwezo wake wa kipekee wa kutawala eneo la kiungo, kupiga pasi zenye usahihi mkubwa na kusoma mchezo kwa kiwango kinachoonekana kuzidi umri wake.
Chole alikuwa mmoja wa wachezaji muhimu walioiongoza Serengeti Boys kufikia fainali ya AFCON U-17 kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, huku akionesha ukomavu mkubwa katika mechi zote muhimu za mashindano hayo. Uwezo wake huo ulimfanya kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mashindano (Man of the Competition), jambo lililomuweka kwenye rada za vilabu kadhaa vya Ulaya.
Inaelezwa kuwa idara ya usajili ya Olympique de Marseille imevutiwa na uwezo wake wa kucheza k**a kiungo wa kati mwenye jukumu la kujenga mashambulizi, huku pia akiwa na uwezo wa kusaidia majukumu ya ulinzi. Sifa hizo zimeonekana kuwa nadra kwa mchezaji wa umri wake na zimeifanya Marseille kuamini kuwa anaweza kuwa mmoja wa wachezaji wakubwa wa baadaye katika soka la Afrika.
Mbali na Marseille, taarifa zinaeleza kuwa vilabu vingine viwili kutoka Ulaya vinaendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo ya kiungo huyo wa Fountain Gate, lakini Marseille ndiyo klabu ambayo imeonekana kuwa mbele zaidi katika mbio za kutaka kupata huduma zake.